KILIMO ni uti wa mgongo wa taifa.
Kauli mbiu hiyo imechangia kuweka mikakati mingi ya kuendeleza kilimo sambamba
na kauli mbiu tofauti kama, ‘Siasa ni Kilimo’, ‘Kilimo Kwanza’ na ‘kilimo cha
kufa na kupona’. Kwa misingi hiyo, Watanzania hawawezi kukwepa suala la kilimo
kwa vile bado ni njia kuu ya kujenga uchumi wa taifa na kuharakisha maendeleo
ya mmoja mmoja.
Kilimo cha mtu mmoja mmoja vijijini mpaka sasa hakijaleta mafanikio makubwa
kutokana na kutumia zana duni ingawa wakulima wachache wamekiri kupata
mafanikio. Wakulima wengi wadogo hawajapata mafanikio kwa kuwa Serikali
haijaweka mikakati madhubuti ya kulima kisasa na kuwatafutia masoko.
No comments:
Post a Comment